Social Icons

Monday, September 5, 2016

YALIYOJIRI KATIKA MKUTANO WA PILI WA NCHI 7 ZA AFRIKA MASHARIKI DHIDI YA MAPAMBANO TOKOMEZA TRAKOMA


Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa ya Kupambana na Trakoma (ITI) akizungumza na washiriki wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma kuhusu uendelezaji wa juhudi za kuwaelimisha wananchi na kutoa tiba katika maeneo  yanakabiliwa na ugonjwa Trakoma kwa nchi washiriki wa mkutano huo kutoka Kenya, Tanzania, Uganda, Ethiopia, Eritrea, Sudani na Sudani Kusini.

Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Upendo John Mwingira akiwasilisha kuhusu mkakati wa kukabiliana na Trakoma kwa kuyafikia maeneo yasiyofikika kirahisi ya jamii za wafugaji nchini Tanzania wakati Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo  unaofanyika  jijini Arusha. Wananchi kutoka Jamii za wafugaji kutoka nchi washiriki wa mkutano huo bado wanakabiliwa na changamoto ya ugonjwa wa Trakoma.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Frida Mokiti akichangia wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma jijini Arusha.

No comments:

 
 
Blogger Templates