Social Icons

Wednesday, July 13, 2016

FC VITO YAINGIA ROBO FAINALI , MICHUANO YA KOMBE LA HELSINKI 2016

 Wachezaji wa timu ya Vito FC wakiwa katika picha ya pamoja
 Wachezaji wa timu ya FC mara baada ya kukabidhiwa bendera ya nchi .


Naibu Waziri wa  Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Annastazia Wambura wakati akiwaaga  vijana hao kwenye hafla iliyofanyika kwenye Ukumbi wa mikutano Idara ya Habari MAELEZO, Jijini Dar es Salaam.


NA SALUM MKANDEMBA

Vijana  wadogo kutoka nchini Tanzania wanaoshiriki michuano ya  kuwania Kombe la Helsinki  (Helsinki Cup 2016)  wamefanikiwa kuingia katika duru  ya robi fainali kwenye michuano inayoendelea jijini Helsinki nchini  Finland.

Timu hiyo inayofahamika kwa jina la  FC Vito Malaika, wamesonga mbele  na  kuitikisa michuano hiyo, baada ya  kushinda mechi mbili na kutoka sare , hivyo wamefanikiwa  kutinga robo fainali.

Kutokana na ushindi na sare hizo za , FC Vito Malaika yenye maskani yake  Nachingwea Mkoani Lindi, imefikisha jumla ya pointi 14 na kusimama kileleni mwa msimamo wa Kundi B G11 la michuano hiyo inayoshirikisha vijana chini ya miaka 16 kutoka mataifa 15 duniani.

Katika mechi zilizochezwa  Jumanne, FC Vito ambayo ni timu ya soka la wanawake, ilianza kwa kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Kopse  katika mechi waliyocheza asubuhi , kabla ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 katika mechi  iliyopigwa  dhidi ya Lluja zote za Finland.

Moto wa FC Vito inayomilikiwa kwa ushirikiano baina ya Sports Development Aid (SDA) ya Tanzania na LiiKe Finland, uliendelea katika mechi zilizochezwa  leo asubuhi , ambako ilianza kwa ushindi wa 4-0  dhidi ya HooGee/KungFu Pandat valkoinen.

Katika mechi ya mchana, FC Vito wakaishia kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya HJK-J/city pia ya hapa, matokeo yaliyoifanya kufikisha pointi 14, tatu juu ya HJK-J/city na TuPs-Japs YJ2. FC Vito imetikisa nyavu mara 22 na kufungwa mabao mawili katika mechi sita ilizocheza.

Kwa mujibu wa ratiba ya michuano hiyo, iliyotolewa na mtandao wa Helsinkicup.torneopal.fi FC Vito Malaika itashuka dimbani kesho kucheza robo fainali na mshindi wa nne wa kundi A G11, linalojumuisha timu saba, ambazo hadi tunaenda mitamboni zilikuwa hazijamaliza mechi zao.

No comments:

 
 
Blogger Templates