Social Icons

Wednesday, July 20, 2016

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA-AfDB YAIPIGA JEKI TANZANIA DOLA MILIONI 200

 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na  Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou, baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya pande hizo mbili, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali kiasi cha shilingi 433.6bn.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (Kulia), akiwa katika picha ya pamoja  na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou (kushoto), Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (wa pili kushoto) na Mwakilishi Mkazi wa AfDB, Tania Kandiero (wa tatu kushoto), baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya pande hizo mbili, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn.Picha Zote na Wizara ya Fedha na Mipango
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb), akipeana mkono na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika -AfDB, Tania Kandiero, alipotembelea Makao Makuu ya Wizara hiyo Jijini Dar es salaam, kwa mazungumzo maalumu, akiwa na Makamu wa Rais wa Benki hiyo, Dkt. Alberic Kacou, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (Kushoto), akimsikiliza kwa makini  Makamu wa Rais wa Benki hiyo, Dkt. Alberic Kacou (katikati) aliyeambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo nchini Tanzania, Tania Kandiero (kulia) ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn. Aliyeketi kushoto ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb)
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Kushoto) akibadilishana "Business Card"  na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou, baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya pande hizo mbili, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, akifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb), na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou (hawapo pichani) ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb), (Katikati), akiwa katika mazungumzo maalumu na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou, katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi yake Jijini Dar es slaam, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn
 Kaimu Kamisha Fedha za Nje kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Mamelta Mtagwaba akifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb), na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou (hawapo pichani), ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Kushoto) akibadilishana "Business Card"  na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou, baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya pande hizo mbili, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akiwa katika mazungumzo maalumu na ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, ukiongozwa na  Makamu wa Rais wa Benki hiyo, Dkt. Alberic Kacou, aliyeambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo nchini Tanzania, Tania Kandiero, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (Kushoto) akizungumza jambo wakati alipokutana na ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, ukiongozwa na  Makamu wa Rais wa Benki hiyo, Dkt. Alberic Kacou (katikati) aliyeambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo nchini Tanzania, Tania Kandiero (kulia) ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn.


Na Benny Mwaipaja-WFM 

Benki  ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, imeahidi kuchangia Dola Milioni 200, sawa na Shilingi 433.6b, kwenye Mfuko wa Bajeti Kuu ya Serikali katika kipindi cha mwaka wa Fedha 2016/2017. 

Ahadi hiyo imetolewa na Makamu wa Rais wa Benki hiyo anayeshughulikia Utawala na Rasilimali watu, Dkt. Alberic Kacou, alipomtembelea Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Ofisini Kwake Jijini Dar es salaam 

Makamu huyo wa Rais wa AfDB aliyeambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo, Tania Kandiero, amesema kuwa mchango huo umeongezeka kwa dola Milioni 50 ikilinganishwa na Bajeti ya mwaka jana ambapo Benki hiyo ilichangia Dola Milioni 150. "Misaada na mikopo inayotolewa na Benki yetu kwa serikali ya Tanzania imefikia Dola za Marekani 1.9b hivi sasa" Alieleza Dkt. Kacou 

Ameeleza kuwa Tanzania ni nchi inayoongoza katika Bara la Afrika kupewa kiasi kikubwa cha fedha kutokana na mipango yake mahili ya maendeleo inayokidhi vigezo na viwango vya taasisi hiyo. "Tuna malengo matano ambapo tunataka kuwekeza katika sekta ya nishati, uzalishaji wa chakula, kuiendeleza kiviwanda, kuiunganisha na kuboresha maisha ya waafrika kwa ujumla" aliongeza Dkt. Kacou 

Amepongeza jitihada zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, kwa kusimamia vizuri nidhamu ya matumizi ya fedha za umma na kwamba uamuzi huo utaharakisha maendeleo ya nchi. Akizungumza na ujumbe huo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, ameshukuru uamuzi wa Benki hiyo wa kuongeza mchango wake katika Bajeti Kuu ya serikali kupitia mfuko mkuu wa Bajeti (GBS). 

Amesema kuwa serikali imedhamiria kutekeleza mipango yake ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge), pamoja na kununua ngege tatu za abiria ili kuboresha usafiri wa anga. 

"Vilevile tumeamua katika Bajeti ya mwaka huu kununua meli mpya itakayo tumika kutoa huduma Ziwa Viktoria na kukarabati meli nyingine mbili ambapo moja iko Ziwa Tanganyika na nyingine Ziwa Viktoria ili kuimarisha usafiri wa majini" Aliongeza Dkt. Mpango 

Dkt. Mpango amebainisha kuwa katika kutekeleza Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo, serikali imejipanga kukuza sekta ya viwanda ili kuiwezesha nchi kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. "Mpango huo utakwenda sambamba na kuboresha sekta ya kilimo ili malighafi itakayozalishwa na wakulima, licha ya kuinua uchumi wa wakulima wetu, lakini pia viwanda vitapata malighafi ya kutosha" alisisitiza Dkt. Mpango 

Amerejea msimamo wa serikali kuwa haitakubali kupokea misaada inayoambatana na masharti magumu na isiyo na tija kwa nchi na kwamba jitihada zinazofanyika hivi sasa ni kuhakikisha kuwa rasilimali zilizopo nchini zinawekezwa kwa utaratibu mzuri ili ziweze kutumika kuleta maendeleo. 

"Hatutakubali misaada isiyozingatia vipaumbele vyetu na ile inayohatarisha uhuru wetu wa kujiamulia mambo yetu wenyewe" alieleza Dkt. Mpango.Ameeleza kuwa uamuzi wa serikali wa kukusanya mapato yake ya ndani kwa kuwahimiza watu kulipa kodi na kubana matumizi yasiyo ya lazima umeanza kuleta matunda na kuongeza pia nidhamu ya matumizi ya pesa katika jamii. 




Ameiahidi Benki hiyo ya maendeleo ya Afrika-AfDB, kwamba fedha waliazoahidi kuzitoa zitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa. 
Click here to Reply, Reply to all, or Forward 14.29 GB (95%) of 15 GB used Manage Terms - Privacy Last account activity: 4 hours ago Details 31 more Ahmad Michuzi's profile photo Ahmad Michuzi Show details

No comments:

 
 
Blogger Templates