Social Icons

Friday, June 17, 2016

WASHINDI WA SHINDANO LA AJIRA YANGU BUSINESS PLAN COMPETITION WAPEWA ZAWADI ZAO JIJINI DAR


Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bing’i Issa, wa kwanza kushoto na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kazi Duniani Mary Kawar, wa kwanza kulia, wakimkabidhi mfano wa cheki yenye thamani ya fedha za kitanzania 15,323,000/=kijana Gilbert Tarimo wa Inoge Rabbit Farm baada ya kuibuka mshindi namba moja kwa wajasiriamali wanaoanza katika shindano la michanganuo ya kibiashara lijulikanalo kama Ajira Yangu lililoratibiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ushirikiano na Shirika la Kazi Duniani (ILO). Shindano hilo lilihusisha zaidi ya michanganuo ya kibiashara 800 kutoka kwa vijana mbalimbani nchini .
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi Bing’i Issa, wa kwanza kushoto na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kazi Duniani Mary Kawar, wa kwanza kulia, wakimkabidhi mfano wa cheki yenye thamani ya fedha za kitanzani kijana Linda Nasson baada ya kuibuka mshindi namba nne kwa wajasiriamali wanaokua katika shindano la michanganuo ya kibiashara lijulikanalo kama Ajira Yangu lililoratibiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ushiriano na Shirika la Kazi Duniani (ILO). Shindano hilo lilihusisha zaidi ya michanganuo ya kibiashara 800 kutoka kwa vijana mbalimbani nchini
Mgeni Rasmi Beng’i Issa, Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) akitoa hutuba wakati wa sherehe za kugawa zawadi kwa washindi wa shindano la Ajira Yangu siku ya Jumatatu ya tarehe 13/06/2016. Kongamano hilo liliandaliwa kwa pamoja na Baraza la Taifa la Uwwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ushirikiano na Shirima la Kazi Duniani (ILO) .

 Dr. Mary Kawar, Mkurugenzi Mkazi, Shirika la Kazi Duniani (ILO) akiongea na vijana (hawapo pichani) pamoja na wageni waalikwa wakati wa ufunguzi rasmi wa sherehe za kutoa zawadi kwa washindi wa shindano la kuandaa michanganao ya kibiashara lijulikanalo kama Ajira Yangu. Sherehe hizo zilifanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na kukutanisha Zaidi ya vijana 400 kutoka mikoa mbalimbali nchini. Kongamano hilo liliandaliwa kwa pamoja na Baraza la Taifa la Uwwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ushirikiano na Shirima la Kazi Duniani (ILO).


 Paul Mashauri, mjasiriamali na mwanzilishi wa Masterclass Worldwide (wa  kwanza kushoto) Mercy Kitomari, mjasiriamali na mwanzilishi wa NELWA Gelato ( katikati) na Immaculate Steven, mjasiriamali na mwanzilishi wa Lavender Catering ( wa kwanza kulia) wakisikiliza kwa makini maswali kutoka kwa vijana wakati wa kongamano la Ajira Yangu lililofanyika katika hoteli ya Serena siku ya tarehe 13/06/2016. Kongamano hilo liliandaliwa kwa pamoja na Baraza la Taifa la Uwwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ushirikiano na Shirima la Kazi Duniani (ILO) .
Dr. Sebastian Ndege, mjasiriamali na Mkurugenzi wa Ndege Insurance Brokers (wa kwanza kushoto), Modesta Lilian Mbughuni, mjasiriamali na mwanzilishi wa The Professional Approach Group (katikati) na Ruge Mutahaba, Mkurugenzi wa Clouds Media Group wakijadili mada katika kongamano la Ajira Yangu lililofanyika katika hoteli ya Serena juni 13 2016

No comments:

 
 
Blogger Templates