Social Icons

Wednesday, June 15, 2016

DAMIAN SOUL , SAVE THE CHILDREN WASHIRIKIANA KUTUNGA WIMBO WA KUMTETEA MTOTO




Damian Soul akiwa  na Mkurugenzi wa Save The Children  Sharon Kassahu.

Msanii  Damian  Inocent Mihayo 'Soul'  kesho Juni 16,inayoadhimishwa kimataifa atazindua wimbo wake ambao ameurekodi maalum kwa ajili ya kupigania haki za watoto unaokwenda kwa jina la 'Watoto wetu' , kuhusu kuacha kuwachapa  watoto  viboko shuleni.

"Nimetoa wimbo huu maalum kwa ajili ya kuenzi siku ya mtoto wa Afrika ambayo inaadhimishwa kesho 

Soul pia amepata fursa ya kufanya kazi na 'Ubongo Kids'  kupitia vikatuni venye sauti na kucheza (Annimation).

Aisha kesho ikiwa ndiyo siku ya Mtoto Duniani  atakuwa Uwanja wa Jakaya Kikwete ulipo maeneo ya Kidongo  Chekundu, Gerezani  ambako atazindua rasmi video hiyo.

"Ujumbe uliopo kwenye wimbo ni  kuhusi haki za watoto na  kusoma bila kuchapwa viboko" alisema Soul. 

Nyimbo hiyo itakuwa ikirushwa kupitia kipindi cha 'Ubongo Kids'  kinachorushwa na kituo cha luninga cha TBC  ili wazazi waweze kuona na kuufanyia kazi hasa waalimu , ambao wamekuwa katika smstari wa mbele kuchapa wanafunzi wanapokuwa wakiwafundisha.

"Waalimu wafanyie kazi  kuwa watoto wanapaswa kufundishwa kuandika na kuchora bila kuchapwa fimbo na kupewa adhabu zinazowaachia maumivu" alisema.

Miwsho anawashukuru  Save the Children ambao ndiyo wamemwezesha kufanikisha kurekodi wimbo guo katika Audio na Video ikiwa ni pamoja na kuandika  baadhi ya maneno kwenye wimbo huo.

No comments:

 
 
Blogger Templates