Social Icons

Saturday, February 6, 2016

DOKTA MANYAUNYAU ALIA KUKIMBIWA NA WATEJA WAKE WAPYA NA WAZAMANI WAKIHOFIA UTAPELI

Dokta Manyaunyau  katika pozi .

Na Mwandishi wetu , Dar es Salaam 

Mdau wa  masuala ya mbalimbali ya burudani  ,muziki  , filamu na sanaa mbalimbali  nchini ambaye pia ni mganga wa tiba za asilia  Jongo Selemani almaarufu kwa jina la ‘Dk Manyaunyau  amejitokeza hadharani kujisafisha juu ya kuchafuliwa jina lake kuwa kafungwa jela.

Akizungumza na Bongoweekend maeneo ya Mlimani City , jijini Dar es Salaam   hivi karibuni alisema kwamba kutumika vibaya kwa  jina lake kumemleta usumbufu mkubwa ikiwa ni pamoja na kukimbiwa na wateja wake wapya  na wa zamani wakimhofia kwamba  yeye ni tapeli jambo ambalo halina ukweli wowote.

“Mimi niko uraiani na sina tuhuma zozote ilitokea tu mtu akawa anafanya shughuli zake akatumia jina langu kwa makosa mimi jina hili nimelisajili na ninalilipia kodi hivyo inauma sana kuona mtu mwingine analitumia kwa maslahi yake binafsi sasa ona ameniletea matatizo makubwa nimekimbiwa na wateja wangu ” alisema Mnayaunyau.

“Awali nilipuuzia na kuona kwa sababu wale watu ambao walikuwa washitakiwa katika  kesi iliyokua ikiunguruma katika mahakama ya Ilala , alikana  kuwa  yeye hakujipa jina hilo  la 'Manyaunyau' bali alipewa na wateja wake aliokuwa akiwatibu.Lakini kusema kweli hivi sasa kashfa hiyo inanigharimu sana” alisema Manyaunyau huku akionesha sura yenye huzuni kwa mwandishi.

Aliongeza kwa kusema kuwa anawasihi wateja  pamoja na mashabiki wake kuwa yeye bado yupo katika ofisi zake zilizopo Tabata Mawenzi  na anaye mhitaji anaweza kumfuata na atapata huduma kama kawaida.Manyaunyau amekuwa mdau mkubwa wa sanaa kutokana na kutoa ufadhili na kuwasaidia wasanii wengi katika nyanja mbalimbali kwa lengo la kuinua sanaa nchini.

No comments:

 
 
Blogger Templates