Social Icons

Thursday, August 27, 2015

KAMATI YA MISS TANZANIA YA KINA LUNDENGA OUT, PINTO JOKATE MWEGELO NDANI



NA MWANDISHI WETU, MAELEZO

SIKU chache baada ya shindano la kumsaka Mrembo wa Tanzania kutoka kwenye kifungo cha Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) uongozi wa Hashim na wenzake wameachia ngazi kupisha uongozi mpya wa mpito.

Akizunguma  leo asubuhi  katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Idara ya Habari (MAELEZO), Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International ambaye pia alikua  Mratibu kwa kipindi cha miaka 21 Hashi Lundenga alisema , “tumekuja hapa leo ikiwa ni katika kutangaza majina mapya ya Kamti ya Miss Tanzania ambao kuanzia sasa watakuwa wakiratibu shindano hilo.
Sisi tutakuwa nyuma yao  hivyo anomba waandishi wa habari muendelee kuwapa ushirikiano wa kutosha.

Lundenga aliitaja kamati hiyo kuwa ni majina na cheo kwenye mabano Juma Pinto (Mwenyekiti wa muda) na Lucas Rutta (Makamu wa Mwenyekiti), Doris Mollel  (Katibu Mkuu) na Jokate Mwegelo (Msemaji wa Kamati),
Wengine ni katika nafasi ya wajumbe ambao aliyekuwa Miss Tanzania 1999 Hoyce Temu, Mohammed Bawazir, Gladyz Shao, Shah Ramadhan, Hamm Hashim , Khalfan Saleh na Ojambi Masaburi.

Aidha kwa upande wa  sekretarieti  wamowajumbe wanne ambao ni Dk. Ramesh Shah, Hidan Ricco aliyekuwa Ofisa Habari wa Lino, Yasson Mashaka na  Deo  Kapteni.
“Hii ndiyo timu yetu ya wachapa kazi  ambao tumewakabidhi jukumu  hili la kuandaa, kusimamia na kuratibu  mashindano ya urembo ya Miss Tanzania.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa majina hayo Pinto alisema kwamba anahidi kulibadilisha shindano hilo ambalo linapendwa na wengi hivyo amehitaji muda ili waweze kujipanga ikiwemo hatma ya ushiriki wa Miss Tanzania Lilian Kamazima kwenye fainali za shindano la kumsaka mrembo wa dunia zitakazo fanyika nchini China baadaye mwaka huu.

“Suala la kushiri kwa mrembo wetu tutalitolea ufafanuzi baada ya wiki mbili pia nina imani majibu yatakuwa mazuri siku ikifika” alisema Pinto.

Jibu hilo la pinto lilikuja baada ya kuulizwa hatma ya ushiriki wa Miss Tanzania ambapo Lundenga alikiri kwamba hawataweza kumuanda kutokana na kuwa nyuma ya muda wa maandalizi pamojana na ukosefu wa fedha pia.

Pinto aliendelea kwa kusema kwamba ndiyo kwanza wamekabidhiwa ofisi leo hivyo wanahitaji kukaa ofisini na kukabidhiwa  rasmi ndipo watajua wapi pa kuanzia.

Wakati huohuo Mwegelo alizungumza kwamba anampongeza Lundenga kwa kukubali kuachi kituia mbacho amekitumikia kwa muda mrefu kwani siyo jambo rahisi.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa watakutana na Basata ili waweze kuzungumza na kufahamishana lipi la kufanya na lipi wasilifanye na baada ya hapo ndipo watakapotoka na uamuzi kama shindano lifanyike mwaka huu ama wasubiri hadi ifikapo mapema mwakani.

Pia ametoa wito kwa wasichana ambao walipoteza matumaini na imani ya mashindano ya urembo kwa kusema kuwa anawatoa hofu kwani hakuna  jambo lililoharibika hivyo wakati ukifika wajitokeze kwa wingi.

“Natoa wito kwa wasichana kuwa waondoe hofu kwani hapa wako kwenye mikono salama” alisema.

Viongozi wa Lino ambao umelazimika kupisha na kufanya mabadiliko ni pamoja na aliyekuwa wake Katibu Bosco Majaliwa, 

 Mkuu wa Itifaki Albert Makoye, Hidan Rico Ofisa Habari na Yasson Mashaka aliyekuwa Mjumbe. 

No comments:

 
 
Blogger Templates