Social Icons

Sunday, January 25, 2015

DAHU WA CLOUDS FM ASHEREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA AMANA HOSPITALI

HUSNA ABDUL 'DAHU' akizungumza na waandishi wa habari nje ya Wodi ya  watoto katika hospitali ya Amana ambako alizaliwa  miaka kadhaa iliyopita. 

MSANII  Zuwena Muhammed  (Shilole), jana alikuwa kivutio tosha katika wodi ya watoto wachanga katika hospitali ya Amana Jijini Dar es Salaam leo asubuhi.

Shilole aligeuka kuwa kivutio baada ya kuwa akiitwa na kina mama waliojifungua na kutaka abebe watoto wao na kupiga nao picha.

Aidha msanii huyo alifika hospitalini hapo akiwa ameambatana na msafara wa Balozi wa watoto wa kuanzia umri wa kuzaliwa hadi miaka mitano Husna Abdul ‘Dahu’ ambaye ni mtangazaji wa kituo cha Clouds FM aliyekuwa akiadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa zawadi kwa watoto wachanga na vifaa tiba kwa hospitali katika kitengo hicho.

Aidha Shilole ametangaza rasmi kumuunga mkono Dahu katika kazi zake za kijamii ambapo atakuwa msanii wa kwanza kumuunga mkono  katika kila hatua ya ubalozi wake kwa watoto  hao hospitalini hapo.

 “Hili ni fundisho tosha kwa wasanii na hata watu wengine katika jamii tubadilike sasa tuwe tunaadhimisha siku kwa namna ya kufanya mrejesho katika jamii kama alivyofanya Dahu amenigusa sana na mimi nitafanya hivyo nitakwenda Igunga siku yangu ikifika” alisema  Shilole.

Aidha shilole aliweza kubeba watoto kadhaa katika wodi hiyo ya watoto na akampa mtoto mmoja jina lake la ‘Shishi Baby’ huku akimsisitiza mama wa binti huyo mchanga ampe na aitunze picha waliyopiga sambamba na la ‘ShishiBaby’.

“Nilizaliwa tarehe 25 Januari 1986 katika hospitali hii ya Amana hivyo  nimeona leo ikiwa ni siku yangu ya kuzaliwa nije kushereheka kwa namna nyingine  kabisa kuwaona watoto wachanga ambao wamezaliwa tarehe kama yangu na kuwapa zawadi wazazi  na kutoa msaada wa vifa tiba” alisema Dahu.

Dahu alizungumza hayo leo  wakati akikabidhi vifaa hivyo  vyenye  thamani yash. Mil.1 ambavyo pia vimetolewa kwa  msaada wa kituo cha Clouds FM.

Muuguzi wa wodi hiyo ambaye Mwanaidi Msai alisema watoto waliozaliwa  ni 37  huku 20 wakike na 17 wa kiume .

Pia wamemshukuru Dahu kwa kujitoa na kuwaomba wasanii wengine waliozaliwa katika hospitali hiyo akiwemo Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’  na viongozi mbalimbali waliozaliwa katika hospitali ya Amana wafike kuwasalimia katika hospitali waliyozaliwa.
 
 Dahu akikabidhi vifaa hivyo  leo.

No comments:

 
 
Blogger Templates