Social Icons

Monday, March 31, 2014

WINDHOEK AMBAO NI WADHAMINI WAKUU WA SHEREHE YA KUTIMIZA MIAKA 3 YA BONGO MOVIE



 Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steve Mengele (Nyerere) akihojiwa na waandishi wa habari wakati wa sherehe ya Kutimiza miaka 3 ya Klabu ya Bongo Movie, sherehe iliyofanyika katika Ukumbi wa East 24 uliopo Katika Jengo la Arcade Mikocheni, Mwishoni mwa Wiki
Warembo wakiwa wamebeba Chupa za Windhoek zinazosambazwa na kuuzwa na Kampuni ya Mabibo Beer ambao ndio walikuwa wadhamini wakuu wa Sherehe ya Kutimiza Miaka 3 ya Klabu ya Bongo inayoongozwa na Steve Nyerere.
Mwenyekiti wa Makampuni yaliyo chini ya Proin Group Of Companies, Bw Johnson Lukaza akipokea cheti cha kuthaminiwa kutoka kwa Mwenyekiti wa Bongo Movie kama mmoja wa wamiliki wa kampuni ya usambazaji wa kazi za filamu nchini  iitwayo Proin Promotions Limited.
 Burudani pia zilikuwepo
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Mabibo Beer, Mama Benadetha Rugemalila akiongea na waandishi wa habari wakati wa sherehe hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa East 24 uliopo Mikocheni katika jengo la Arcade.
 First lady wa B Band inayoongozwa na Baba Zoro
 Wadau wakifuatilia burudani safi kutoka kwa wasanii mbalimbali waliopanda kwenye jukwaa
 Warembo wa Bongo Movie wakiingia ukumbi tayari kwa Kufurahia Miaka 3 ya Kuzaliwa kwa Bongo Movie.
 Nuruel akiendelea kuimba kwa hisia katika sherehe hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki
 Mwenyekiti wa Bongo Movie akitoa maneno kwa wageni waalikwa pamoja na wasanii wa bongo movie na muziki nchini waliohudhuria sherehe hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa East 24.
 Keki ikikatwa kama ishara ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Bongo Movie ikiwa imetimiza miaka 3
 Rich Rich akilishwa keki na Mwenyekiti
 Mwenyekiti wa Makampuni yaliyochini ya Proin Group of Companies, Bw Johnson Lukaza akihojiwa na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa sherehe ya kutimiza miaka 3 ya kuzaliwa kwa Bongo Movie.
 Bi Mwenda akifurahi kukabidhiwa cheti cha sifa ya kuwa msanii mkongwe
 Mtitu akipokea Cheti kutoka Kwa Mwenyekiti.
 Hawa ndio mabalozi wa Windhoek waliochaguliwa katika sherehe hiyo ya kutimiza miaka 3 ya bongo movie.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mabibo Beer, Mama Benadetha Rugemalila ambae alikuwa mdhamini mkuu wa sherehe hiyo kupitia kampuni ya Mabibo Beer akitoa maneno mawili matatu mara baada ya mabalozi wa Bia ya Windhoek kuchaguliwa
 Amin Akishusha Burudani 
 Linex akiimba kwa hisia
 Shilole hakuwa nyuma na wimbo wake wa chuna buzi
Christa Bela akitoa vionjo safi kabisa katika sherehe hiyo.

No comments:

 
 
Blogger Templates